• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Tanzania Rural and Urban Roads Agency-TARURA
Tanzania Rural and Urban Roads Agency-TARURA

Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
  • Miradi na Programu
    • Project and Program
    • RISE - MAY- 2021
    • TeRMIS
  • Utawala
    • Kurugenzi ya Barabara
      • Sehemu ya Barabara Vijijini
      • Sehemu ya Barabara Mijini
    • Kurugenzi ya Mipango na Miundombinu
      • Sehemu ya Usalama Barabarani
      • Sehemu ya Mipango na Miundombinu ya Barabara
    • Kurugenzi ya Huduma Saidizi
      • Sehemu ya Rasilimali Watu na Utawala
      • Sehemu ya Mipango, Ufuatiliaji na Tathimini
    • Kitengo cha Uhasibu
    • Kitengo cha Tafiti na Udhibiti Ubora
    • Kitengo cha Teknlojia ya Habari na Takwimu
    • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
    • Kitengo cha Ununuzi
    • Kitengo cha Huduma za Sheria
    • Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano
    • Kitengo cha Mazingira na Maendeleo ya Jamii
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Bajeti na Taarifa za Mapato
    • Fomu Mbalimbali
    • Majarida
    • Vipeperushi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video
    • Habari
    • Matukio
    • Maktaba ya Picha
  • Manunuzi
    • Taarifa ya Manunuzi
    • Zabuni za Wazi
    • Tuzo za Zabuni
  • Mitandao ya Barabara
    • Mitandao ya Barabara za Tarura
  • Mikoa
    • Mameneja wa Mikoa
    • Mameneja wa Wilaya

MHE. JAFO ARIDHISHWA NA UJENZI WA BARABARA YA UHURU

Posted on: March 6th, 2021

MHE. JAFO ARIDHISHWA NA UJENZI WA BARABARA YA UHURU

Na. Thereza Chimagu, Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani S. Jafo (Mb), ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa Barabara inayoingia Hospitali ya Uhuru kwa kiwango cha lami yenye urefu wa Mita 320 kwa njia mbili ambayo inasimamiwa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma.

Waziri Jafo alitoa pongezi hizo alipokuwa akifanya ziara ya ukaguzi wa miradi mbalimbali mkoani Dodoma Machi 03, 2021 na kuoneshwa kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa Barabara hiyo.

“Tumejenga Hospitali ya Uhuru lakini sehemu hii ya kuingilia ilikuwa na changamoto kubwa, nimekuja hapa kuangalia maendeleo ya ujenzi wa barabara hii na kwa kweli nimeridhika kuona maendeleo ya ujenzi wa barabara hii”, alisema Mhe. Jafo.

Aidha Mhe. Jafo alimtaka Mkandarasi anayetekeleza ujenzi wa barabara hiyo M/S Nyanza Co. Ltd kutumia muda uliopo ili kuweza kukamilisha mradi kwa wakati kutokana na changamoto za mvua zinazoendelea kunyesha.

Akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa Barabara hiyo, Meneja wa TARURA Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Mhandisi Nelson Maganga alisema kuwa ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami umefikia asilimia 85 na tayari lami nyepesi imekamilika kwa ajili ya kuweka tabaka la lami nzito.

“Ujenzi wa Barabara umefikia asilimia 85 kukamilika na tunatarajia Mkandarasi kumaliza kazi kulingana na mkataba kufikia Machi 14, 2021, sehemu hii ya barabara imegharimu kiasi cha shilingi Milioni 511”, alisema Mhandisi Nelson.

Katika hatua nyingine Mhe. Jafo alifanya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa Barabara za Mji wa Serikali Mtumba kwa kiwango cha lami zenye urefu wa Km 51.2 na kuonesha kutoridhishwa na kasi ya Mkandarasi anayetekeleza ujenzi wa barabara hiyo Kampuni ya China Heinan International Cooperation Co. Ltd (CHICO) na kumtaka Mkandarasi huyo kuhakikisha anamaliza ujenzi kama ilivyo kwenye Mkataba ifikapo Julai 30, 2021.

“Sijaridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa mradi huu kuwa chini ya asilimia 6, leo hii mpo asilimia 63 na mlitakiwa muwe asilimia 69 mimi nilikuja hapa nikijua mpo asilimia 70, sihitaji mjadala wa aina yeyote ninachotaka mradi huu uwe umekamilika kama ilivyo kwenye makubaliano”, alisema Mhe Jafo.

Akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa Barabara za Mji wa Serikali Mtumba, Mkurugenzi wa Barabara za Mijini TARURA, Mhandisi Mohamed Mkwata alisema kuwa Mkandarasi amefikia asilimia 63 za maendeleo ya jumla ya utekelezaji wa Mradi ambapo alitakiwa kuwa asilimia 69, ameongeza kuwa ujenzi wa tabaka la lami umefikia Km 11.2, uwekaji wa lami nyepesi Km 15.7, ujenzi wa tabaka la pili umefikia Km 15.7, ujenzi wa tabaka la kwanza umefikia Km 15.7, ujenzi wa mifereji Km 6.6, pamoja na ujenzi wa vivuko 64 dhidi ya 130 vinavyohitajika.

Aidha, Mhandisi Mkwata alieleza kuwa katika kipindi cha mwezi Novemba 2020 uhaba wa Saruji pamoja na mvua zinazoendelea kunyesha zilisababisha baadhi ya kazi kusimama na kufanya Mkandarasi kuwa nyuma ya asilimia 6 za utekelezaji wa Mradi na kuongeza kuwa ili kufidia muda uliopita Mkandarasi ameongeza mitambo ili kuweza kumaliza mradi huo kwa wakati uliopangwa.

Mhe. Jafo amefanya ukaguzi katika Barabara ya Mji wa Serikali Mtumba ikiwa ni ziara yake ya tatu kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo inayosimamiwa na TARURA na mradi unatarajiwa kukamilika ifikapo Julai 30,  2021.

Matangazo

  • INVITATION FOR TENDERS - DODOMA June 08, 2022
  • TANGAZO LA KAZI -KAGERA April 21, 2022
  • CALL FOR INTERVIEW - MTWARA January 17, 2022
  • CALL FOR AN INTERVIEW - MWANZA December 23, 2021
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • TARURA YASAINI MIKATABA YA MABILIONI KUIMARISHA MTANDAO WA BARABARA VIJIJINI NA MIJINI

    August 14, 2022
  • MAAGIZO 10 YA RAIS SAMIA KWA TAMISEMI NA TARURA

    August 14, 2022
  • WANANCHI KILOSA WAFURAHIA UJENZI DARAJA LA BEREGA

    August 12, 2022
  • RAIS SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KM 40 MUFINDI, IRINGA

    August 11, 2022
  • Angalia zote

Video

Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Barua pepe za Watumishi - TARURA
  • Mfumo wa Maegesho (TeRMIS)
  • Lipia Maegesho (TeRMIS)
  • Mfumo wa eMrejesho

Tovuti Muhimu

  • Wakala wa Barabara
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • OR-TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Wizara ya Ujenzi uchukuzi na mawasiliano
  • Utumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Baraza la Mitihani
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • Instragram_tarura
  • twitter_tarura
  • Mfumo wa Maegesho (TeRMIS)
  • Mfumo wa eMrejesho

Waliotembelea duniani

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    TANZANIA RURAL AND URBAN ROADS AGENCY (TARURA),TARURA HOUSE GOVERNMENT CITY -MTUMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 11042, DODOMA

    Simu ya mezani: 026-2963846

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ceo@tarura.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Waliotembelea

StatCounter

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati Miliki @2017 TARURA. Haki zote zimehifadhiwa