• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Tanzania Rural and Urban Roads Agency-TARURA
Tanzania Rural and Urban Roads Agency-TARURA

Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
  • Miradi na Programu
    • Miradi iliyo kamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyochini ya Ununuzi
    • Project and Program
    • RISE - FEB- 2021
  • Utawala
    • Kurugenzi ya Huduma na Uendeshaji
    • Kurugenzi ya Barabara za Vijijini
    • Kurugenzi ya Barabara za Mijini
    • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
    • Kitengo cha Huduma za Sheria
    • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
    • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
    • Kitengo cha udhibiti Ubora na Utafiti
    • Sehemu ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano(TEHAMA)
    • Sehemu ya Utawala na Rasilimali Watu
    • Sehemu ya Mipango
    • Waratibu wa Mikoa
    • Mameneja wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Bajeti na Taarifa za Mapato
    • Fomu Mbalimbali
    • Majarida
    • Vipeperushi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video
    • Habari
    • Matukio
    • Maktaba ya Picha
  • Manunuzi
    • Taarifa ya Manunuzi
    • Zabuni za Wazi
    • Tuzo za Zabuni
  • Mitandao ya Barabara
    • Mitandao ya Barabara za Tarura
  • Mikoa
    • Waratibu wa Mikoa
    • Mameneja wa Halmashauri

TARURA YAPONGEZWA UJENZI WA DARAJA LA KANKWALE MKOANI RUKWA

Posted on: December 8th, 2020

TARURA YAPONGEZWA UJENZI WA DARAJA LA KANKWALE MKOANI RUKWA

Na. Erick Mwanakulya, Rukwa.

Wananchi wa Kata ya Senga Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, mkoani Rukwa wameipongeza Serikali kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwa ujenzi wa Daraja la Kankwale linalounganisha Sumbawanga Asilia na Kankwale.

Naye, Mkazi wa Mtaa wa Katambazi Bw. Erod Kastiko ameishukuru Serikali kwa ujenzi wa daraja hilo kwani litakuwa kiunganishi kikubwa kwa wakazi wa Sumbawanga Asilia pamoja na Kankwale na litarahisisha shughuli za maendeleo pamoja na shughuli za usafiri na usafirishaji.

“Tunaishukuru sana TARURA kwa ujenzi wa daraja hili, hapo awali tulikuwa na daraja lakini kutokana na mvua nyingi, daraja hilo lilisombwa na maji na kusababisha kero kwetu sisi wakazi wa Katamba na vijiji vyote vya jirani, hivyo ujenzi wa daraja hili utatusadia katika suala la usafiri na usafirishaji”, alisema Bw. Erod.

Meneja wa TARURA Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, Mhandisi Seleman Mzirai alisema kuwa ujenzi wa daraja hilo ulianza mapema mwezi Januari 2020 na unatarajiwa kukamilika mwezi Januari 2021, ila kutokana na kasi ya Mkandarasi ujenzi huo utakamilika mapema mwezi Desemba 2020.

“Ujenzi wa daraja hili umefikia asilimia 70 kukamilika, kazi zinazoendelea ni ujenzi wa kuta za pembeni ili kuweza kuzuia mmomnyoko wa udongo, daraja hili litasaidia sana wakazi wa maeneo haya katika shughuli zao za usafiri na usafirishaji na hasa kipindi cha mvua kwani litapitika kipindi chote”, alisema Mhandisi Mzirai.

Aidha, mbali na ujenzi wa daraja hilo katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, TARURA Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi imetekeleza mradi wa Barabara za Lami zenye urefu wa Km 2.9 ambazo zimekamilika kwa asilimia 100 huku ujenzi wa barabara ya lami yenye urefu wa Km 1 katika barabara ya Ikulu ambayo ni mradi wa Ahadi za Mhe. Rais ukiwa umekamilika.

Naye, Meneja wa TARURA Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi, Mhandisi Elly Jonas Mkwizu alieleza kuwa Mji wa Namanyere kwa sasa unapendeza baada ya kujenga barabara za lami na kwamba mabadiliko yatakuwa makubwa katika Wilaya hiyo baada ya miradi mbalimbali iliyopo katika hatua za utekelezaji kukamilika.

“Namanyere kwa sasa inabadilika, barabara hizi za lami zimeufanya mji upendeze na tunaendelea kuomba bajeti ya kutosha ili tutekeleze miradi mingine walau sehemu kubwa ya mji wetu iwe na barabara za lami”, alisema Mhandisi Mkwizu”.

Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) katika Mkoa wa Rukwa unaendelea kutatua kero mbalimbali za wananchi kwa kujenga madaraja ili kuunganisha maeneo mbalimbali ya Mkoa huo, ikiwemo ujenzi wa daraja la Kavunja katika Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi ambalo limefikia asilimia 45 kukamilika ili kuunganisha Kata ya Kirando na kata ya Korongwe ikiwa ni pamoja na kurahisisha shughuli za kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa maeneo hayo.

Matangazo

  • INVITATION FOR LOGO DESIGN COMPETITION November 12, 2020
  • SHINDANO LA KUANDAA NEMBO (LOGO) YA TARURA-KISWAHILI November 12, 2020
  • WALIOITWA KWENYE USAILI KADA YA UDEREVA TARURA MKOA WA TANGA November 06, 2020
  • KUITWA KWENYE USAILI-KIGOMA October 30, 2020
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MHE. JAFO ARIDHISHWA NA UJENZI WA BARABARA YA UHURU

    March 06, 2021
  • DARAJA LA MWASONGE KUUNGANISHA MISUNGWI NA NYAMAGANA

    February 22, 2021
  • TARURA INAVYOBORESHA MIUNDOMBINU MKOA WA RUVUMA

    February 18, 2021
  • TARURA INAVYOENDELEA KUTATUA KERO KWA WANANCHI MKOANI DODOMA

    February 03, 2021
  • Angalia zote

Video

Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Tarura Barua pepe za Watumishi

Tovuti Muhimu

  • Wakala wa Barabara
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • OR-TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Wizara ya Ujenzi uchukuzi na mawasiliano
  • Utumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Baraza la Mitihani
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • Instragram_tarura
  • twitter_tarura

Waliotembelea duniani

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    TANZANIA RURAL AND URBAN ROADS AGENCY (TARURA),TARURA HOUSE GOVERNMENT CITY -MTUMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 11042, DODOMA

    Simu ya mezani: 026-2963846

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ceo@tarura.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Waliotembelea

StatCounter

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati Miliki @2017 TARURA. Haki zote zimehifadhiwa